Loading...

Machapisho

Taarifa /Machapisho

TAARIFA


  • Ukumbusho wa Uwajibikaji

    ( 16 February, 2024)

  • Kikao cha Watumishi Wote

    (18 January, 2024)

  • HATI ya Zabuni

    (30 August, 2023)

MACHAPISHO


  • Sheria za Mlo Kamili.

  • Dalili za Malaria.

  • Elimu ya Malezi

KALENDA


  • Siku ya Macho Duniani

    (10 Oktoba)

  • Siku ya Uchangiaji Damu Duniani

    (14 June)

  • Siku ya Lishe Duniani

    (16 Oktoba)

  • Siku ya Ukimwi Duniani

    (01 December)

VIKAO


  • Vikao SME Watumishi

    ( Jumatano)

  • Kikao cha Watumishi Wote

    (Mwisho wa Robo Mwaka)

  • Kikao HMT

    (Mwisho wa Robo Mwaka)

Taarifa

Kambi Maalum ya Madaktari Bingwa wa Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassani , ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha. Tarehe: 20-24/05/2024

Hii ni Kambi Maalum ya Madaktari Bingwa wa Mheshimiwa Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassan ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha iliyoandaliwa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa Wataalamu wa Afya ndani ya Tanzania. Kambi ilienda vizuri ikiambatana na ushirikiano wa hali ya juu kutoka kwa washiriki walioweza kufika.

Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha. Tarehe: 17/05/2024

Haya ni Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Hospitali ya Jiji Arusha yakijumuisha Wauguzi mbalimbali wanaopatikana ndani ya Jiji la Arusha. Maadhimisho yalienda vizuri yakiambatana na Maandamano ya kuvutia.

Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano TANZANIA ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha. Tarehe: 26/04/2024

Maadhimisho ya Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA) yakijumuisha Wakazi, watumishi mbalimbali pamoja na viongozi mbalimbali yakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Felician Mtahengera kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha katika kushiriki shughuli mbalimbali zikiwemo Zoezi la Utoaji Damu, Upandaji wa Miti, ushauri wa masuala ya Afya pamoja na Ufanyaji usafi mazingira kuzunguka Hospitali ya Jiji la Arusha.

Ujio wa Timu Kazi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU ) ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha. Tarehe : 04/02/2024

Lilikuwa ni tukio la kuvutia ambapo Timu Kazi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU )walifika katika Hospitali ya Jiji Arusha kuunga mkono jitihada za Hospitali yetu katika zoezi zima la utoaji wa huduma za Afya katika jamii. Zoezi lilienda vizuri likiandamana na upandaji wa Miti ya kuvutia ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha

Kikao cha Asubuhi ( Morning Report) cha Wafanyakazi wa Hospitali ya Arusha Jiji

Hiki ni kikao cha Wafanyakazi wa Hospitali ya Arusha Jiji kinachofanyika Mara Nne ( Kwa siku Nne) kila Wiki kuzungumzia changamoto Mbalimbali za Kiutendaji wanazokutana nazo wafanyakazi. Pia, kikao hiki hutumiwa na wafanyakazi katika kushirikishana mawazo ya kujenga katika zoezi la utoaji huduma kwa wagonjwa.

Kliniki ya Mama na Mtoto, Hospitali ya Arusha Jiji. Tarehe: 23/02/2024

Hii ni huduma ya Kliniki ya Mama na Mtoto inayotolewa na kitengo cha Uzazi wa Mpango ( RCH ) Muda ni Kila Siku, kuanzia saa 02:00 Asubuhi hadi Saa 09:30 Mchana ikiwa na lengo la kufuatilia na kuhakikisha Maendeleo ya Mama na Mtoto katika jamii yanazingatia vigezo vinavyotakiwa na Wizara ya Afya. Pia huduma hii inahakikisha Maendeleo ya mtoto baada ya kuzaliwa yanakuwa vizuri ikijumuisha pia huduma za Ushauri wa uzazi wa Mpango kutoka kwa wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Arusha Jiji

Zoezi la Uelimishaji jamii kuhusu Lishe, Radio TBC Arusha. Tarehe: 24/01/2024

Hili ni zoezi lililoandaliwa na radio TBC Arusha kwa kushirikiana na Wataalmau wa Afya ya Lishe kutoka Hospitali ya Arusha Jiji. Zoezi lilikuwa na lengo la kutoa elimu kwa jamii kuhusu kanuni bora za Lishe katika kujikinga na magonjwa mbalimbali. Zoezi lilifanyika vizuri na jamii ilifanikiwa kupata elimu kuhusu Afya ya Lishe kupitia Radio TBC Arusha

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Arusha Jiji, Dkt. Salma Kitara akikagua Ujenzi unaoendelea wa Jengo la Wagonjwa wa Nje, Hospitali ya Arusha Jiji. Tarehe: 19/02/2024

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Arusha Jiji, Dkt. Salma Kitara akikagua Ujenzi unaoendelea wa jengo linalotazamiwa kutumika kwa ajili ya Wagonjwa wa Nje katika Hospitali ya Arusha Jiji. Kwa ripoti inayoonesha kuwa Ujenzi unaendelea vizuri katika kuboresha Miundombinu ya Utoaji huduma kwa Wagonjwa

Mkuu wa Mkoa wa Arusha. Mhe. John Mongella akikagua Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje, Hospitali ya Arusha Jiji. Tarehe: 18/10/2023

Mkuu wa Mkoa wa Arusha akikagua ujenzi wa jengo la wagonjwa wa Nje unaonedelea katika Hospitali ya Arusha Jiji. Ujenzi unaendelea vizuri ikiwa ni Matazamio ya Hospitali hiyo kuimarisha miundombinu rafiki ya ufanyaji kazi kwa huduma za wagonjwa wa nje kutoka kwa wataalamu wabobezi wa Afya katika hospitali hiyo

Kliniki ya Mama na Mtoto. Muda : Kila siku, Saa 02:00 Asubuhi - Saa 09:30 Alasiri

Hii ni huduma ya Kliniki ya Mama na Mtoto inayotolewa na kitengo cha Uzazi wa Mpango ( RCH ) Muda ni Kila Siku, kuanzia saa 02:00 Asubuhi hadi Saa 09:30 Mchana ikiwa na lengo la kufuatilia na kuhakikisha Maendeleo ya Mama na Mtoto katika jamii yanazingatia vigezo vinavyotakiwa na Wizara ya Afya. Pia huduma hii inahakikisha Maendeleo ya mtoto baada ya kuzaliwa yanakuwa vizuri ikijumuisha pia huduma za Ushauri wa uzazi wa Mpango kutoka kwa wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Arusha Jiji

Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya SURUA / RUBELLA kwa Watoto. Tarehe : 15 - 18 /02/2024

Hii ni kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya SURUA / Rubella kwa watoto wa umri kuanzia Umri wa Miezi Tisa hadi Umri wa Miaka Mitano ikiwa na lengo la kuhakikisha Mtoto anapata kinga ya magonjwa ya Surua na RUBELLA ambayo yanaathiri afya ya Mtoto katika makuzi. Huduma hii ilitolewa na wataalamu wetu wabobezi katika Hospitali ya Arusha Jiji kwa ufanisi wa hali ya juu ikipata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wazazi wa watoto waliowaleta katika Hospitali ya Arusha jiji

Uanzishwaji wa Mfuko wa Mama na Mtoto Hospitali ya Arusha Jiji

Huu ni mkakati na utekelezaji wa malengo ya Wizara ya Afya katika kuhakikisha Afya ya Mama na Mtoto baada ya kujifungua inazingatiwa na kupatiwa uangalizi mzuri. Zikiwemo pia huduma za kukidhi mahitaji muhimu ya Mama mjamzito baada ya kujifungua ili kuimarisha Afya ya mtoto.

Kikao cha Mpango wa Mwaka Hospitali ya Arusha Jiji

Hiki ni kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Vikao wa Hospitali ya Arusha Jiji ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mipango ya utekelezaji wa shughuli za utoaji Huduma za Afya kwa jamii

Matukio

Hospitali ya Arusha Jiji imeratibu Matukio mbalimbali yanayoendana na Taaluma zao katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ndani na nje ya maeneo ya Hospitali katika kuhakikisha huduma bora za Afya kwa jamii. Miongoni mwa matukio ni pamoja na;

Image

Tarehe : 19/02/2024

Mganga Mfawidhi akikagua Ujenzi unaondelea wa Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD Complex)

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Arusha Jiji, Dkt. Salma Kitara akikagua Ujenzi unaoendelea wa jengo linalotazamiwa kutumika kwa ajili ya Wagonjwa wa Nje katika Hospitali ya Arusha Jiji. Kwa ripoti inayoonesha kuwa Ujenzi unaendelea vizuri katika kuboresha Miundombinu ya Utoaji huduma kwa Wagonjwa. Hali ya ujenzi inaendelea vizuri, ikiwa ni Maboresho katika Miundombinu ya utoaji Huduma za Afya kwa wagonjwa wanaofika kupata huduma.

Peruzi zaidi
Image

Tarehe : 18/10/2023

Mkuu wa Mkoa wa Arusha. Mhe. John Mongella akikagua Ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Nje, Hospitali ya Arusha Jiji

Mkuu wa Mkoa wa Arusha akikagua ujenzi wa jengo la wagonjwa wa Nje unaonedelea katika Hospitali ya Arusha Jiji. Ujenzi unaendelea vizuri ikiwa ni Matazamio ya Hospitali hiyo kuimarisha miundombinu rafiki ya ufanyaji kazi kwa huduma za wagonjwa wa nje kutoka kwa wataalamu wabobezi wa Afya katika hospitali hiyo. Ujenzi unaendelea vizuri kwa ufanisi wa Wahandisi mahiri wa Ujenzi ikizingatiwa kufikia malengo na ubora wa Hospitali ya Arusha Jiji katika kuimarisha mazingira bora ya utoaji wa huduma kwa Wagonjwa wanaofika kupata huduma za Afya.

Peruzi zaidi
Image

Tarehe : 27/01/2024

Uchangiaji Damu Ndani ya Eneo la Halmashauri ya Arusha Jiji

Hili ni Tukio lilifanyika ndani ya eneo la Halmashauri ya Arusha Jiji lililoratibiwa na Wataalamu Wabobezi wa Afya kutoka Hospitali ya Arusha Jiji likiwa na lengo la kuendesha zoezi la Uchangiaji damu pia kuendesha utoaji wa Huduma za Elimu ya Afya kwa jamii ikiwa na dhumuni la kuimarisha uelewa wa jamii juu ya magonjwa mablimbali na namna ya kujikinga na magonjwa hayo yanayosumbua jamii

Peruzi zaidi
Image

Tarehe : 17/12/2023

Semina ya Mafunzo ya Huduma za Afya ndani ya ofisi za Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC). Njiro, Arusha

hii ni Semina ya Mafunzo ya Huduma za Afya zilizofanyika katika ofisi ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) yenye lengo la kutoa Elimu ya Afya pamoja na kuongeza uelewa kwa jamii juu ya namna ya kujikinga na magonjwa mbalimbali yanayosumbua katika jamii. Semina hii iliongozwa na wataalamu wetu wabobezi kutoka Hospitali ya Arusha Jiji

Peruzi Zaidi
Image

Tarehe: 14/11/2023

Semina ya ushauri wa Afya ndani ya ofisi za VETA, Njiro Arusha

Hii ni Semina ya ushauri wa huduma za Afya iliyoendeshwa na Wataalamu wetu wa Afya kutoka Hospitali ya Arusha Jiji yenye lengo la kutoa ushauri wa masuala ya Afya na namna ya kuimarisha elimu ya kujikinga na magonjwa mbalimbali katika jamii. Ni Semina yenye tija kwa jamii ndani ya Mkoa wa Arusha

Peruzi Zaidi
Image

Tarehe: 14/11/2023

Semina ya ushauri wa Afya ndani ya ofisi za VETA, Njiro Arusha

Hii ni Semina ya ushauri wa huduma za Afya iliyoendeshwa na Wataalamu wetu wa Afya kutoka Hospitali ya Arusha Jiji yenye lengo la kutoa ushauri wa masuala ya Afya na namna ya kuimarisha elimu ya kujikinga na magonjwa mbalimbali katika jamii. Ni Semina yenye tija kwa jamii ndani ya Mkoa wa Arusha

Peruzi Zaidi
Image

Tarehe : 20/10/2023

Ujio wa Katibu Mkuu Taifa wa TUGHE ndani ya Hospitali ya Arusha Jiji

Huu ulikuwa ni wakati mzuri kwa Watumishi wa Hospitali ya Arusha Jiji kuwa na mazungumzo yenye tija na Katibu wa TUGHE Taifa ambapo Mgeni rasmi alihimizia Umoja na Mshikamano kwa wafanyakazi katika kuimarisha utoaji wa Huduma bora kwa wagonjwa wanaofika ndani ya Hospitali ya Arusha Jiji kupata huduma mbalimbali

Peruzi Zaidi
Image

Tarehe : 04/09/2023

Kikao cha Mafunzo cha SME Kwa Watumishi wa Hospitali ya Arusha Jiji

Hiki ni Kikao cha Mafunzo ambacho hufanyika katika Ukumbi wa Vikao wa Hospitali ya Arusha Jiji kikiwa na lengo la kufundishana, kubadilishana mawazo na kuchambua njia sahihi za kutumia katika kutatua changamoto mbalimbali za Kiafya wanazokutana nazo watu katika jamii. Kanzi Nzuri Timu !!.

Peruzi Zaidi
Image

Tarehe: 30/09/2023

Kikao cha Mganga Mfawidhi Dr. SALMA KITARA na Wafanyakazi Wote

Hiki ni Kikao hufanyika katika Ukumbi wa Vikao katika Hospitali ya Arusha Jiji ambapo Mwenyekiti wa Kikao hiko alikuwa Mganga Mfawidhi kuzungumzia maboresho yanayotakiwa yafanyike katika kuimarisha huduma za Afya kwa wagonjwa wanaofika katika Hospitali ya Arusha Jiji

Peruzi Zaidi
Wadau Wetu

Tafadhali Andika Maoni Yako

Tafadhali Andika Maoni Yako Hapa kwa Ajira ya Kuboresha Huduma. Karibu sana!!