Loading...

Huduma za Meno & Uzazi

Huduma za Meno & Uzazi

Hospitali ya Arusha Jiji inajumuisha Huduma mbalimbali za Matibabu zinazotolewa kwa wagonjwa wanaofika hospitali. Huduma hizi hutolewa na Wataalamu wetu wabobezi wa Masuala ya Afya. Huduma hizi ni kama zifuatazo;

1. HUDUMA YA KLINIKI YA MENO

Hospitali ya Arusha Jiji ina wataalamu Wabobezi katika Huduma ya Kliniki ya Meno kwa wagonjwa mbalimbali katika jamii. Baadhi ya Huduma ya matibabu ya Meno ni kama zifuatazo;

  • Tunatengeneza Meno Bandia
  • Crown and bridge
  • Orthodontic Removable Applinces
  • Mouth Guards
  • Tooth Gems / Tooth Jewely
  • Veneers
  • Dental X-Ray
  • Oral Screen
  • Habits Breaker
  • Flexible Denture

Miongoni mwa Takwimu za Huduma ya Kliniki ya Meno inayotolewa katika Hospitali ya Jiji la Arusha kutoka kwa wataalamu wetu wabobezi inajumuisha zifuatazo;

Kitengo / Mwaka
2021 (Wagonjwa)
2022 (Wagonjwa)
2023 (Wagonjwa)
2024 (Wagonjwa)
Chini Miaka 5 14 27 115 156
Chini Miaka 14 30 42 95 61
Zaidi Miaka 15 74 62 83 119

Hospitali ya Jiji la Arusha inatoa Huduma za Kliniki ya Meno kutoka kwa wataalamu wetu wabobezi. Huduma bora kwa kuzingatia utaalamu wa kutosha ili kuleta matokeo bora kwa wapokea huduma kutoka kwetu


2. HUDUMA YA UZAZI

Hospitali ya Arusha Jiji ina wataalamu Wabobezi katika Huduma ya Uzazi Macho kwa wagonjwa mbalimbali katika jamii. Baadhi ya Huduma za Uzazi zinazopatikana katika Hospitali ya Arusha jiji ni pamoja na zifuatazo;

  • Huduma za Operation
  • Huduma ya Mama na Mtoto
  • Huduma ya Ushauri Uzazi wa Mpango

Miongoni mwa Takwimu za Huduma za Uzazi zinazotolewa katika Hospitali ya Jiji la Arusha kutoka kwa wataalamu wetu wabobezi zinajumuisha kama ifuatavyo;

Kitengo / Mwaka
2021 (Wagonjwa)
2022 (Wagonjwa)
2023 (Wagonjwa)
2024 (Wagonjwa)
Wajawazito 1483 3831 3881 964
Wagonjwa wa Nje (OPD) 9887 20828 29016 7859
Wazazi 174 1148 1653 410

Huduma ya Uzazi inatolewa katika Hospitali ya Jiji la Arusha kwa wapokea Huduma wote mara Kabla na Baada ya kujifungua kwa ubora wa hali ya juu kutoka kwa wataalmau wetu wabobezi ili kuhakikisha huduma bora zinatolewa kulingana na viwango vinavyohitajika na Wizara ya Afya Tanzania.


Tafadhali Andika Maoni Yako

Tafadhali Andika Maoni Yako Hapa kwa Ajira ya Kuboresha Huduma. Karibu sana!!