Mafunzo ya Matibabu kwa Watu wasioona ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Haya ni Mafunzo ya Matibabu kwa Watu wasioona ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha kwa watumishi wote wa Hospitali ya Jiji Arusha. Mafunzo yaliyoandaliwa na kitengo cha Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Wataalamu wabobezi wa masuala ya Walemavu wasioona. Mafunzo yalienda vizuri yakiwa na lengo la kuboresha utoaji wa huduma ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Maadhimisho kuelekea Siku ya Wauguzi Duniani, 12 Mei 2026 ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa wa Arusha International Conference Centre (AICC)
Ni maadhimisho ya kuelekea Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano jijini Arusha, Arusha International Conference Centre (AICC).Maadhimisho ambayo yalifunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Dkt. Toba Nguvila. Sisi kama timu ya Hospitali ya Jiji Arusha tunayo furaha kuhudhuria maadhimisho haya yenye kuonesha kuthamini mchango wa Wauguzi katika kutoa huduma za afya kwa jamii
Semina Mafunzo Elekezi juu ya Matumizi ya Mfumo wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Taarifa za Watu wenye Ulemavu (PD-MIS) mkoani Arusha
Mafunzo yaliyoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kuwakutanisha Wataalamu mbalimbali kutoka ofisi hiyo na Maafisa Ustawi wa Jamii na wadau mbalimbali wa utoai wa huduma za kijamii. Afisa Ustawi wetu wa Hospitali ya Jiji la Arusha Miss Renatha Tesha ambae ni mmoja wa wahudhuriaji wa mafunzo hayo yaliyolenga uboreshaji wa utoai wa huduma kwa watu wenye Makundi Maalumu katika jamii
Zawadi za Wafanyakazi Bora wa Mwaka 2026 Siku ya Wafanyakazi (MEI MOSI)
Hospitali ya Jiji Arusha ina furaha sana kutambulishwa kwa wafanyakazi bora wa Mwaka 2026 ambao ni watumishi wetu ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha, Miss NIWAEL SUMARI (Muuguzi Mfawidhi wa Jiji), Miss ESTHER PIUS (Afisa Lishe) na Ndugu DENIS SINKALA (Mtaalamu wa Dawa za Usingizi) wakiwa ni sehemu ya waliopatiwa zawadi ya utumishi bora wa umma katika sherehe za Siku ya wafanyakazi zilizofanyika ndani ya Halmashauri ya Jiji la Arusha. Hongereni sana watumishi wenzetu.
Semina Elekezi ya Mafunzo kwa vijana wa Shule za Sekondari juu Masuala ya Ustawi wa Jamii ndani ya Halmashauri ya Jiji la Arusha
Semina ikiwa ni miongoni mwa mikakati inayofanywa na Maafisa Ustawi wetu katika kuhakikisha jamii inapata uelewa wa kutosha juu ya masuala yanayohusu Ustawi wa Jamii ikiwa ni pamoja na jamii kutambua nafasi zao katika kutokomeza vitendo vyenye kuvunja haki za binadamu
Kikao kazi cha Viongozi wa Hospitali na Bodi ya Usimamizi wa Hospitali ya Jiji la Arusha
Hiki ni kikao kazi kati ya uongozi wa Hdspitali ya Jiji Arusha na Kamati ya Bodi ya usimamizi wa Shughuli za Hospitali ya Jiji Arusha ikiwa ni moja ya mikakati ya kuboresha huduma za afya katika jamii. Kikao kilienda vizuri kikiwa na dhumuni kubwa la utekelezaji wa maadhimio mbalimbali yaliyowekwa
Ziara ya Diwani wa Kata ya Engutoto Mh. Hamza Njiku ya Hospitali ya Jiji la Arusha
Ujio wa Diwani wa Kata ya Engutoto Mheshimiwa Hamza Njiku ndani ya Hospitali ya Jiji la Arusha ikiwa ni sehemu ya ujio wa kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na namna ya kuboresha huduma za Afya katika hospitali ya Jiji la Arusha. Ziara ilienda vizuri ikiambatana na majidiliano mbalimbali na wafanyakazi wa Hospitali ya Jiji la Arusha
Mafunzo ya Elimu ya Afya (CME) yaliyofanywa na Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Muriet Dkt. Noel ndani ya Hospitali ya Jiji la Arusha
Mafunzo haya ikiwa ni sehemu ya kukumbushana na kuboresha utoaji wa huduma za Afya katika Halmashauri ya Jiji la Arusha. Mafunzo yalienda vizuri na kuhudhuriwa na watumishi wote wa Hospitali ya Jiji la Arusha
Mafunzo ya Elimu ya Afya (CME) yaliyofanywa na Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Muriet Dkt. Noel ndani ya Hospitali ya Jiji la Arusha
Mafunzo haya ikiwa ni sehemu ya kukumbushana na kuboresha utoaji wa huduma za Afya katika Halmashauri ya Jiji la Arusha. Mafunzo yalienda vizuri na kuhudhuriwa na watumishi wote wa Hospitali ya Jiji la Arusha
Mafunzo ya Dharura kwa akina Mama na Watoto Wachanga katika Hospitali ya Jiji Arusha
Haya ni Mafunzo ya Dharura kwa Watoa Huduma za Afya kwa akina Mama na Watoto Wachanga katika masuala ya kuhakikisha Huduma bora za Uzazi zinatolewa kwa wagonjwa wanaokuja kupata huduma katika Hospitali ya Jiji Arusha. Mafunzo yalienda vizuri katika kuwaongezea uwezo wataalamu wa Afya katika jamii
Mafunzo ya Dharura kwa akina Mama na Watoto Wachanga katika Hospitali ya Jiji Arusha
Haya ni Mafunzo ya Dharura kwa Watoa Huduma za Afya kwa akina Mama na Watoto Wachanga katika masuala ya kuhakikisha Huduma bora za Uzazi zinatolewa kwa wagonjwa wanaokuja kupata huduma katika Hospitali ya Jiji Arusha. Mafunzo yalienda vizuri katika kuwaongezea uwezo wataalamu wa Afya katika jamii
Sherehe ya Watumishi Kupeana Zawadi (Get Together) ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Ni Sherehe iliyoandaliwa na Kamati ya Matukio ya Kijamii (Social Arusha City Hospital) ikiwa na lengo la kuimarisha Umoja, Upendo na Ushirikiano kwa wafanyakazi wote ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha ili kuboresha uwajibikaji wakati wa kutoa huduma kwa wagonjwa ndani ya hospitali yetu.
Semina Mafunzo Elekezi ya Afya ya Mama na Mtoto ndani ya Hospitali ya Jiji la Arusha
Hii ni Semina elekezi ikiwa ni sehemu ya Mafunzo juu ya Afya ya Mama na Mtoto kabla na baada ya kujifungua. Semina ambayo iliendeshwa na wataalamu wa Afya kutoka Hospitali ya Jiji Arusha ikiambatana na watumishi wa afya kutoka katika vituo mbalimbali vya Afya ndani ya Jiji la Arusha
Kampeni ya Usafi wa Jiji la Arusha ndani ya Hospitali ya Jiji
Ni moja ya Kampeni za kuhakikisha jiji la Arusha linakuwa safi kwa kuhusisha wadau mbalimbali wa maendeleo. Zoezi ambalo liloongozwa na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Arusha Joseph Mkude
Ugeni wa Mkuu wa Wilaya ya Arusha ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Moja ya ugeni wenye tija kubwa kwa jamii katika kuhakikisha miradi inayoendelea kufanyika ndani ya hospitali ya Jiji Arusha, ukiwemo mradi wa Ujenzi wa Jengo la wagonjwa wa Nje (OPD) Complex ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Joseph Mkude akiambatana na timu yake ndani ya viwanja vyetu vya hospitali
Maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la OPD Complex ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Ni moja ya sehemu inayoonesha maendeleo ya Ujenzi wa Jengo la OPD Complex ndani ya Hospitali ya jiji Arusha ikiwa ni moja ya maagizo ya serikali katika kuimarisha huduma za afya ndani ya jiji la Arusha
Ugeni wa Benki ya NCBA ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha kama mdau wa Huduma za Afya
Ulikuwa ni muda mzuri kuikaribisha timu ya Benki ya Benki ya NCBA ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha, zoezi likiambatana na upandaji wa miti kama ishara ya ushirikiano katika huduma za afya.
Ujio wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha (Mhe. Amos Makalla) ziara ya kutembelea ujenzi wa Jengo la OPD Complex
Ni ziara ya kutembelea ujenzi wa Jengo la OPD Complex ikiwa ni moja ya agizo la serikali katika kuboresha sekta ya Afya kupitia mikikati ya miundombinu na vitendea kazi vya kutolea huduma kwa jamii
Kambi ya Matibabu ya Madaktari Bingwa wa Mhe. Raisi Samia S. Hassan ndani ya Hospitali ya jiji Arusha.
Hii ni kambi ya Matibabu kutoka kwa madakatari bingwa wa Mhe. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa na lengo la kuimarisha uwezo wa wataalamu wetu katika zoezi zima la utoaji wa huduma bora za afya kwa wagonjwa mbalimbali ndani ya hospitali ya Jiji Arusha
Mganga Mfawidhi, Dr. Said A. Salim akikagua Ujenzi unaoendelea wa Jengo la OPD Complex ndani ya Hospitali ya jiji Arusha
Mganga Mfawidhi Dr. Said A. Salim akifanya Ukaguzi wa Ujenzi unaoendelea wa Jengo la OPD Complex ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha ukiwa na lengo la kuimarisha Ufanisi na utoaji wa huduma bora za afya ndani na nje ya halmashauri ya Jiji la Arusha kwa jamii
Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi ndani ya Hospitali ya jiji Arusha
Hii ni sherehe ya Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi iliyofanyika ndani ya Hospitali ya jiji Arusha ikiambatana na maandamano ya Wauguzi mbalimbali ndani ya Jiji la Arusha. Tukio lilienda vizuri na kufurahiwa na watoa huduma wengine mbali na wauguzi
Kliniki ya Mama na Mtoto ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Ni Kliniki ya Mama na Mtoto (RCH) ikiwa ni miongoni mwa huduma zinazopatikana ndani ya hospitali ya Jiji Arusha ambayo hutolewa kila siku kuanzia saa Mbili kamili asubuhi mpaka saa Tisa na Nusu asubuhi katika kuhakikisha ukuaji na afya bora ya mtoto
Utoaji wa Elimu ya Lishe ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Ni zoezi la utoaji wa elimu kuhusu lishe lililoendeshwa na Afisa lishe katika ukumbi wa Hospitali. Zoezi likiambatana na mafunzo ya lishe kwa vitengo miongoni mwa washiriki katika kulinda afya za watoto
Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA) ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Yalikuwa ni Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA) katika viwanja vya Hospitali ya Jiji Arusha ikiambatana na viongozi mbalimbali mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa wilaya ya Arusha Jiji ndugu Mhe. Felician Mtahengerewa shughuli ikiambatana na zoezi la upandaji wa miti pamoja na usafi wa mazingira
Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi ndani ya Hospitali ya jiji Arusha
Hii ni sherehe ya Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi iliyofanyika ndani ya Hospitali ya jiji Arusha ikiambatana na maandamano ya Wauguzi mbalimbali ndani ya Jiji la Arusha. Tukio lilienda vizuri na kufurahiwa na watoa huduma wengine mbali na wauguzi
Ujio wa Timu ya Taasisi na Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha
Ulikuwa ni ugeni wa Timu ya Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndani ya viwanja vya Hospitali ya Jiji Arusha ukiambatan na zoezi zima la upandaji wa miti ikiwa ni alama ya kuonesha umoja na mshikamano katika utoaji wa huduma za Afya katika jamii