Taarifa

Kambi ya Matibabu ya Madaktari Bingwa wa Mhe. Raisi Samia S. Hassan ndani ya Hospitali ya jiji Arusha

Hii ni kambi ya Matibabu kutoka kwa madakatari bingwa wa Mhe. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa na lengo la kuimarisha uwezo wa wataalamu wetu katika zoezi zima la utoaji wa huduma bora za afya kwa wagonjwa mbalimbali ndani ya hospitali ya Jiji Arusha


Mganga Mfawidhi, Dr. Salma Kitara akikagua Ujenzi unaoendelea wa Jengo la OPD Complex ndani ya Hospitali ya jiji Arusha

Mganga Mfawidhi Dr. Salma Kitara akifanya Ukaguzi wa Ujenzi unaoendelea wa Jengo la OPD Complex ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha ukiwa na lengo la kuimarisha Ufanisi na utoaji wa huduma bora za afya ndani na nje ya halmashauri ya Jiji la Arusha kwa jamii

Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi ndani ya Hospitali ya jiji Arusha

Hii ni sherehe ya Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi iliyofanyika ndani ya Hospitali ya jiji Arusha ikiambatana na maandamano ya Wauguzi mbalimbali ndani ya Jiji la Arusha. Tukio lilienda vizuri na kufurahiwa na watoa huduma wengine mbali na wauguzi

Kliniki ya Mama na Mtoto ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha

Ni Kliniki ya Mama na Mtoto (RCH) ikiwa ni miongoni mwa huduma zinazopatikana ndani ya hospitali ya Jiji Arusha ambayo hutolewa kila siku kuanzia saa Mbili kamili asubuhi mpaka saa Tisa na Nusu asubuhi katika kuhakikisha ukuaji na afya bora ya mtoto

Utoaji wa Elimu ya Lishe ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha

Ni zoezi la utoaji wa elimu kuhusu lishe lililoendeshwa na Afisa lishe katika ukumbi wa Hospitali. Zoezi likiambatana na mafunzo ya lishe kwa vitengo miongoni mwa washiriki katika kulinda afya za watoto

Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA) ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha

Yalikuwa ni Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (TANZANIA) katika viwanja vya Hospitali ya Jiji Arusha ikiambatana na viongozi mbalimbali mgeni rasmi akiwa ni Mkuu wa wilaya ya Arusha Jiji ndugu Mhe. Felician Mtahengerewa shughuli ikiambatana na zoezi la upandaji wa miti pamoja na usafi wa mazingira

Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi ndani ya Hospitali ya jiji Arusha

Hii ni sherehe ya Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi iliyofanyika ndani ya Hospitali ya jiji Arusha ikiambatana na maandamano ya Wauguzi mbalimbali ndani ya Jiji la Arusha. Tukio lilienda vizuri na kufurahiwa na watoa huduma wengine mbali na wauguzi


Ujio wa Timu ya Taasisi na Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndani ya Hospitali ya Jiji Arusha

Ulikuwa ni ugeni wa Timu ya Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ndani ya viwanja vya Hospitali ya Jiji Arusha ukiambatan na zoezi zima la upandaji wa miti ikiwa ni alama ya kuonesha umoja na mshikamano katika utoaji wa huduma za Afya katika jamii


Wasiliana Nasi

(+255) 682 136 704

Tuma Ujumbe

ach@arushacc.go.tz

Eneo Tulipo

Njiro, Contenna. S.L.P 3013 Arusha. TANZANIA